Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

NIMR kutafiti magonjwa yasiyoambukiza nchini

DAR ES SALAAM

Na Devotha Mwang’ata

Taasisi ya Taifa ya Tafiti za Magonjwa ya Binadamu (NIMR) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya inatatarajia kuanza kufanya utafiti wa magonjwa yasiyoambukiza kwa njia ya simu ili kuwafikia wananchi wengi.
Njia hiyo itasaidia kuwafikia Watanzania wengi kwa muda mfupi na kuokoa gharama.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Profesa Said Aboud alisema NIMR imechagua njia hiyo ili kuwafikia watu wengi kwa muda mfupi na kwamba suala hilo linawezekana kutokana matumizi ya simu kuwa makubwa nchini.
“Kutokana na ongezeko kubwa la matumizi ya simu za mkononi, NIMR tumeona ni wakati muafaka kutumia simu za mkononi katika ukusanyaji na uchakataji wa takwimu, kwani itakuwa njia rahisi sana na itaweza kukabiliana na vizuizi vya muda mrefu katika ukusanyaji wa takwimu na ufuatiliaji, hii itasaidia upatikanaji wa taarifa muhimu kwa wakati,”alisema Aboud.
Mpango huo utasaidia kufanya tafiti kwa ufanisi wa matumizi ya simu za mkononi kwenye kukusanya taarifa za tafiti nchi nzima na kutuwezesha kuishauri serikali kama matumizi ya tecknolojia yanawezesha upatikanaji wa taarifa sahihi.
Alisema kuwa lengo la kuzungumza na wanahabari ni kuufahamisha umma juu ya kuwepo kwa utafiti huo utakaowashirikisha wanachi moja kwa moja.
Aboud alisema kuwa utafiti huo utajumuisha sampuli ya wananchi wenye umri kati ya miaka 18 na kuendelea na utafanyika Tanzania Bara pamoja na Zanzibar na unategemea kuchukua wiki nne hadi sita.
Kwa upande wake, Dk. Mery Maige Mtafiti kiongozi wa Magonjwa yasiyo ya kuambukiza pia Mtafiti Mkuu Mwandamizi na Mkurugenzi wa Taarifa za Utafiti Taasis ya Utafiti ya Magonjwa ya Binaadamu NIMR amesema kuwa lengo la utafiti huo ni kuangalia hali ya Magonjwa yasiyoambukiza na viashiria vyake kwa njia ya simu .
Aliongeza kwamba utafiti huo utakaokuwa unaangalia viashiria vya magonjwa unatakiwa kufanywa mara kwa mara ili kubaini na mabadiliko ya mwenendo wa maisha unavyoathiri afya za watu.
“Kwa kuangalia hilo tumeona kuwa hatuwezi kufanya tafiti za nyumba kwa nyumba kwa sababu ya gharama na muda na changamoto ya kuwafikia wananchi wengi hivyo kutumia njia ya simu ni nyenzo muhimu ya kufanya utafiti mara kwa kwa mara,” alisema Dk. Maige.
Alisema kuwa ili kudhibiti wahalifu wa mtandaoni watu wataofanyiwa utafiti watatumiwa meseji maalum itakayowafahamisha juu ya kufanyiwa utafiti ili kuepushwa kupigiwa na matapeli.
Takwimu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonesha kuwa magonjwa yasiyoambukiza yaliongezeka mara mbili kutoka asilimia 19 mwaka 1990 hadi asilimia 34 mwaka 2015 na yanakadiriwa kuchangia asilimia 33 ya vifo vyote.
Nchini Tanzania katika kipindi cha Julai 2022 hadi Machi 2023, magonjwa yasiyoambukiza ambayo yamesababisha wagonjwa wengi kuhudhuria vituo vya huduma za Afya ni pamoja na shinikizo la juu la damu wagonjwa 1,456,881 sawa na asilimia 49 ikilinganishwa na asilimia 34 kipindi kama hicho mwaka 2021/22, kisukari wagonjwa 713,057 sawa na asilimia 24 na magonjwa ya mfumo wa hewa 386,018 sawa na asilimia 13 ikilinganishwa na asilimia 10 kwa kipindi kama hicho mwaka 2021/22.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.