Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Washabiki Yanga wavamia mtandao wa Mamelodi

Mashabiki wa Yanga Mashabiki wa Yanga

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Siku chache baadaya kuchezeshwa kwa droo ya Robo Fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika, washabiki mbalimbali wa timu ya Yanga wameibukia kwenye mtandao wa kijamii wa klabu ya Mamelody Sundowns ya Afrika Kusini na kuipiga mikwara.
Machi 12 mwaka huu, Yanga ilipangwa kucheza na mabingwa hao wa Ligi ya Afrika Kusini katika hatua ya Robo Fainali ya michuano hiyo, huku watani zao Simba wakiangukia mikononi mwa Al Ahly ya nchini Misri.
Kupitia ukurasa wa kijamii wa Instagram wa Mamelodi Sundowns ujulikanao kama Sundowns FC, washabiki hao wamefurika kwenye eneo la maoni (comments) na kuitisha miamba hiyo ya Afrika Kusini kwa maneno ya kejeli.
Katika maoni hayo wapo mashabiki walioonyesha kuwakaribisha Tanzania, na wapo ambao waliwatisha kwa kutaja majina ya nyota wao kama vile Aziz Ki, Max Nzengeli, Mudathir Yahya na wengineo.
Washabiki hao waliibuka hasa baada ya Mamelodi kuweka picha katika mtandao huo inayoonyesha kwamba watakutana na Yanga katika hatua hiyo ya Robo Fainali.
“Masandawana out” aliandika shabiki mmoja wa Yanga aitwaye Chollo Chalile, akimaanisha Mamelodi itatupwa nje ya mashindano hayo. Masandawana ni neno la utani la timu hiyo.
Shabiki mwingine aitwaye Amani Eliji, aliandika, “Mnajua kitu kinachoitwa 5G?”
Mikwara hiyo pia imekuwa ikiendelea kutolewa hata pale klabu hiyo ilipochapisha vitu ambavyo havihusiani na mechi yao dhidi ya Yanga, mfano pale walipoweka chapisho la kuwapongeza baadhi ya wachezaji wao walioitwa kwenye timu ya taifa, bado washabiki wa Yanga waliwajia juu na kuwatambia.
Mara ya mwisho timu hizo zilikutana kwenye hatua za awali za michuano ya CAF mwaka 2001 ambapo mchezo wa kwanza Yanga ilifungwa 3-2 ugenini na kisha kulazimishwa sare ya 3-3 nyumbani.
Mchezo wa nyumbani ulichezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Timu hizo zitakutana tena, huku mambo mengi yakiwa yamebadilika kwenye soka ikiwemo muundo wa uongozi na wachezaji wa timu zote mbili.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.