Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Mdau anunua magoli ya Simba, Yanga

Clatus Chama Clatus Chama

GEITA

Na Joel Maduka-Geita

Kufuatia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kuendelea kusaidia kuinua michezo kwa kununua magoli, mdau mmoja wa michezo mkoani Geita, Hussen Makubi amejitokeza na kuongeza dau kwa Simba na Yanga kwa kila goli watakalolifunga kwenye mechi zao za Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika.
Yanga inapambana kuhakikisha inaitoa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini katika hatua ya Robo Fainali huku Simba ikitaka kuondokana na mazoea ya kuishia robo fainali kwa kutaka kuiondosha mashindanoni Al Ahly ya Misri.
Makubi maarufu kama Mwananyanzara ambaye tangu awali alikuwa na utaratibu wa kutoa shilingi laki tano kwa kila goli, sasa amepandisha dau kwa kuahidi kutoa shilingi milioni moja kwa kila goli.
Akizungumza na Tumaini Letu Makubi alisema amesikia Rais Samia amepandisha dau kutoka shilingi milioni tano hadi 10 kwa kila goli kwa timu hizo, hivyo na yeye kwa uwezo wake ameamua kutoka kwenye kiwango cha shilingi laki tano hadi milioni moja.
“Nimepandisha dau kwa kila goli litakalofungwa na Yanga na hata watani zetu Simba nao nitafanya hivyo hivyo.Lengo langu ni kuona timu hizo zinafanya vizuri kimataifa,”alisema Makubi ambaye ni shabiki mkubwa wa Yanga mkoani Geita.
Makubi aliahidi kuchinja ng’ombe na kuwanywesha supu wakazi wa Geita mjini kama ikitokea timu yake ya Yanga ikapata fursa ya kusonga mbele kwenda nusu fainali.
“Tutafunga mitaa Geita yote hii na kushangilia kama Yanga itafanikiwa kuwatoa Mamelodi na kwenda nusu fainali, na nitachinja ng’ombe na kuwanywesha supu mashabiki wote.Ninaamini hata mikoa mingine itaiga kwa hiki ninachokifanya,”alisema Makubi.
Baadhi ya wadau wa soka mkoani Geita akiwemo Emmanuel Ikolongo Otto na Emily Kimamba, wamempongeza Makubi kwa kujitoa kuzipa hamasa timu hizo.
“Mwananyanzala anafanya vizuri kwa sababu anaonyesha kwamba Geita ina wadau wa michezo wanaopenda maendeleo,” alisema Otto.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.