Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Nyumba ya Luis Rubiales kikaangoni

 Luis Rubiales Luis Rubiales

MADRID, Hispania
Watu sita wamekamatwa baada ya ofisi za Shirikisho la Soka la Hispania pamoja na nyumba ya Rais wa zamani wa Shirikisho hilo, Luis Rubiales kuvamiwa na maafisa wa upelelezi kama sehemu ya uchunguzi.
Uchunguzi huo unahusu utakatishaji fedha na rushwa katika kashfa ya kuhamishwa kwa mashindano ya Super Cup ya Hispania kwenda Saudi Arabia.
Hadi sasa nyumba 11 zimepekuliwa juu ya kashfa hiyo inayokadiriwa kuwa na thamani ya pauni milioni 30.
Mamlaka nchini Hispania zimethibitisha kuwa Rubiales ni mmoja kati ya watu wengine watano ambao wameanza rasmi kuchunguzwa.
Maafisa hao hawakufanikiwa kumkuta Rubiales, kwani taarifa zinaeleza kuwa yupo nje ya nchi hiyo.
Ofisi ya waendesha mashtaka wa Serikali ya Hispania imesema kuwa polisi wakishirikiana na wapelelezi wa Europol walikuwa wakitafuta nyaraka fulani.
Ikumbukwe kuwa Rubiales ana kesi nyingine ya kumbusu mchezaji wa timu ya soka ya taifa ya wanawake ya Hispania baada ya fainali za Kombe la Dunia la wanawake zilizofanyika mwaka jana.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.