Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Maana ya ‘FIFA Series’ na utaratibu wake

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Mashindano maalum ya FIFA Series yamekuwa yakiwaacha njia panda Watanzania wengi ambao wamekuwa na maswali mengi hasa pale walipoiona Taifa Stars ikishiriki kule Azerbaijan.
Michuano ya FIFA Series ya 2024 ni msururu wa mechi zinazotambuliwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa FIFA, zinazohusisha timu za taifa kutoka mashirikisho tofauti ya mabara mbalimbali duniani.
Tayari uzinduzi wa mashindano hayo umefanyika mwezi huu ambao umehusisha mechi za makundi matano tofauti, iliyofanyika katika nchi tano mwenyeji kuanzia Machi 21 hadi 26 mwaka huu.
Mashindano hayo ya kirafiki yalitangazwa kwa mara ya kwanza kama mpango wa FIFA mnamo Desemba 2022 yakiwa najina la ‘FIFA World Series’, na baadaye kuthibitishwa na Rais wa FIFA Gianni Infantino mnamo Machi 16,2023 kufuatia kuchaguliwa tena kwa wadhifa huo wakati wa Kongamano la 73 la FIFA. mjini Kigali, Rwanda.
Shindano hili litaleta pamoja timu za taifa za wanaume kutoka mashirikisho yake sita katika msururu wa mashindano ya kirafiki wakati wa dirisha la mechi za FIFA na kufanyika Machi kila mwaka.
Mashindano hayo yananuiwa kuvipa vyama wanachama wa FIFA nafasi muhimu za kucheza kwa kuwaruhusu kucheza mara kwa mara timu kutoka mashirikisho mengine ambayo vinginevyo hawatakabiliana nayo, na hivyo kuruhusu fursa zaidi za maendeleo ya kiufundi.
Kwa mfano kumekuwa na ugumu kwa timu za barani Afrika kukutana na timu za Ulaya hasa kwa kukosa nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mara kwa mara, hivyo FIFA Series hutoa faida kwa timu hizo kukutana.
Inakusudiwa pia kutoa vyama vya wanachama na fursa za ziada za kibiashara na mengine mengi.
Fainali hizo za mwaka 2024 zinafanyikakama hatua ya awali ya majaribio ya shindano hilo.
FIFA Series imegawanywa katika vituo vikuu sita ambavyo ni Algeria, Azerbaijan, Misri, Saudi Arabia A, Saudi Arabia B na Sri Lanka.
Kituo cha Algeria kinahusisha timu kama Algeria, Andorra, Bolivia na South Africa huku cha Azerbaijan kikiwa na timu za  Azerbaijan, Bulgaria, Mongolia na Tanzania.
Kituo cha Misri kina mwenyeji Misri, Croatia, New Zealand naTunisia wakati kituo cha Saudi Arabia A kina timu za Cambodia, Cape Verde, Equatorial Guinea na Guyana.
Saudi Arabia B ina timu za Bermuda, Brunei, Guinea na Vanuatu wakati Sri Lanka ina Bhutan, Central African Republic, Papua New Guinea na wenyeji Sri Lanka.
Mabara sita yaliyounganishwa kupitia FIFA Series ni Afrika(timu tisa), Asia(timu tano), Amerika Kusini(timu moja), Amerika Kaskazini(timu mbili), Oceania(timu tatu) na Ulaya(timu nne).
Katika FIFA Series ya mwaka huu. Misri pekee ndiyo ilikuwa na muundo wa mtoano, huku washindi wakiamuliwa kwa mikwaju ya penalti baada ya sare ndani ya muda wa kawaida.
FIFA Series ya Misri ni tofauti kidogo ambapo yenyewe inajulikana kama Kombe la Soka la Kimataifa la ACUD, ikiwa imefanyika Cairo na Mji Mkuu Mpya wa Utawala mnamo Machi 22, 23 na 26, na imehusisha wenyeji Misri (CAF), Croatia (UEFA), New Zealand (OFC) na Tunisia (CAF).

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.