Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kundi la West Life na harakati zake kimuziki

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Westlife ni kundi la muziki la nchini Ireland, lililoundwa Machi 3 mwaka 1998 na kuvuma duniani kote.
Asili ya kundi hili linajumuisha wanamuziki kama vile Nicky Byrne, Kian Egan, Mark Feehily, Shane Filan na Brian McFadden ambaye ameacha kuimba tangu mwaka 2004.
Kwa sasa Feehily na Filan ndio wanaotumika kama waimbaji wakuu katika bendi hii.
Bendi hii ya Westlife ndiyo bendi pekee katika historia ya muziki wa Uingereza kuwahi kuwa na nyimbo za kwanza saba moja kwa moja hadi namba moja, na pia wameweza kuuza hadi nakala zaidi ya milioni arobaini na tano dunia nzima ambayo inajumuisha nyimbo zilizorekodiwa studio,video, na albamu zenye kujumuisha nyimbo mbalimbali.
Mwaka 2008, walitangazwa kushika nafasi ya tisa wanamuziki matajiri zaidi walio chini ya umri wa miaka 30, na kushika nafasi ya 13, kwa ujumla. Kwa upande wa Uingereza wamekuwa na nyimbo za peke peke yaani singels hadi kumi na nne, na kushika nafasi ya tatu katika histoia ya Uingereza.
Kundi hili la muziki limewahi kuvunja rekodi mbalimbali kama vile, wanamuziki waliowahi kuwa na miziki mingi katika nafasi ya kwanza nchini Uingereza na pia kwa uuzaji mkubwa zaidi katika eneo la Wembley
Katika miaka mingi ya kazi zao,kundi la Muziki la Westlife wamekuwa wakitengeneza nyimbo za vijana maarufu  za aina ya pop na kutilia mkazo katika nyimbo aina ya ballads.
Wanamuziki wote wanaojumuisha kundi hili ni waandishi wa nyimbo. Lakini nyimbo zao nyingi zimeandikwa na waandishi kutoka nje ya kundi lao. Moja kati ya waandishi maarufu waliowahi kutengeneza nyimbo za kundi hili ni pamoja Steve Mac na Wayne Hector.
Juni mosi mwaka 2008, Westlife walifanya maadhimisho ya miaka 10, ambapo walifanya tamasha katika jiji la Dublin katika eneo la Croke Park na ambapo watu zaidi ya 83,000 walihudhuria hafla hiyo maalumu.
ALBAMU YA WEST LIFE
Westlife ni albamu kutoka kwa kundi la Westlife, moja ya albamu iliyofanya vizuri katika maeneo mbalimbali. Albamu hii ilitoka tar.1 Novemba 1999, nchini Uingereza.
Albamu hii pia ilijumuisha single tatu ambazo ni “Swear It Again”, “If I Let You Go” na “Flying Without Wings”, ambapo single zote tatu zilifanikiwa kufika katika nafasi ya kwanza katika chati ya nchini Uingereza.
Albamu hii ilingia katika chati na kushika nafasi ya pili, ikiwa na mauzo ya nakala zaidi ya 83,000, wakati kati ya hizo nakala 1,000 ziliuzwa wakati albamu hii ikiwa katika nafasi ya kwanza. Albamu hii ilikuja kutolewa katika nafasi ya kwanza na wimbo wa “Steptacular” ulioimbwa na Steps.
Albamu hii ilishika nafasi ya nane kwa upande wa mauzo kwa mwaka 1999 nchini Uingereza. Albamu ya Westlife imefanikiwa kuuza nakala zaidi ya milioni nne dunia nzima.
Albamu ya Westlife ilitoka nchini Marekani mwaka 2000, lakini ikiwa na orodha ya nyimbo tofauti na kuongeza wimbo kama “My Private Movie” uliotayarishwa na Cutfather akishirikiana na Joe.
Albamu hii inabaki albamu pekee ya Westlife kuwahi kuingia katika chati ya muziki ya nchini Marekani, ambapo ilishika nafasi ya 129 kati ya nyimbo 200 bora za Billboard.Ilishika nafasi ya 15 nchini Australia. Single ya More Than Words, ilitolewa nchini Brazi na kushika nafasi ya 2.
Mwezi Desemba mwaka huo huo, single za ‘I Have a Dream’ na ‘Seasons in the Sun’ zilishika nafasi ya kwanza kama nyimbo bora za Krismasi kwa mwaka huo, na bado ndizo single zilizowahi kupata mafanikio zaidi katika bendi ya Westlife.
Mwezi Machi mwaka 2000, single ya tano na ya mwisho kutoka katika albamu hii Fool Again ilitoka na kufikahadi nafasi ya kwanza.
Na kwa sababu hii, Westlife wakawa na single tano kutoka katika albamu moja kufika katika nafasi ya kwanza ndani ya mwaka mmoja, rekodi ambayo bado haijavunjwa hadi hii leo.
Albamu hii ilitolewa katika vijiboksi vikiwa na albamu ya Turnaround Januari 25, 2005 huku kukiwa hakuna kilichabadilishwa katika albamu ya kwanza.
WAPARAGANYIKA NA KURUDI UPYA
Kikundi hicho kilisambaratika mwaka wa 2012 baada ya uhai wa miaka 14 na baadaye kuungana tena mwaka wa 2018.
Mnamo Machi 17, 2021, walitangaza rasmi kwamba walitia saini mkataba mpya wa albamu kupitia Warner Music UK na East West Records.
Walitumbuiza kwenye hafla ya BBC Radio 2 kwenye Ukumbi wa Ulster, Belfast mnamo Agosti 25,2021 ambayo ilitangazwa mnamo 10 Septemba 2021.
‘Starlight’, wimbo wa kwanza kutoka kwa albamu yao ya kumi na mbili, ilitolewa tarehe Oktoba  14, 2021. Albamu hiyo, Wild Dreams, ilitolewa Novemba 26, 2021.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.