Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Parokia Kipunguni walilia barabara

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Walei wa Parokia ya Mtakatifu Thomas wa Akwino – Kipunguni, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Yusuph Mkindi ameuomba Uongozi wa Serikali ya Mtaa kuwatengenezea barabara inayotoka Moshi Bar, kuelekea parokiani hapo, kutokana na kuwa kero, hasa kipindi cha mvua.
Mkindi alitoa ombi hilo wakati akizungumza na Tumaini Letu, baada ya Adhimisho la Misa Takatifu ya Dominika ya Matawi iliyoadhimishwa hivi karibuni parokiani hapo.
“Sisi katika Mitaa yetu tuna Viongozi ambao wanaliona hili, na tumeshawaambia, lakini siyo kuwaambia tu, hata wao wenyewe wanaona pia…
“Kwa hiyo, tunaiomba Serikali ya Mkoa, na hata kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, tumwombe pamoja na uongozi wote watuangalie katika barabara hii, kwa sababu Waamini wanashindwa kufika kanisani, hasa mvua kubwa kama hizi za masika zinapoanza,” alisema Mwenyekiti huyo.
Mkindi aliwapongeza Waamini wenzake kwa upendo, umoja na ushirikiano wanaoendelea nao parokiani hapo, hasa katika shughuli mbalimbali za Kanisa.
Aidha, aliwasihi kuendelea kujitolea kwa moyo katika kulijenga Kanisa, huku akiwaasa pia kujitolea kwa moyo kuwasaidia wahiji, hasa katika kipindi hiki cha Kwaresma.
“Tuwaone wahitaji kwamba ni sehemu yetu sisi, kwa hiyo tuwatumikie, tuwape kile ambacho kinawafaa, kwani tukifanya hivyo, Mungu wetu anazidi kutubariki,” alisema Mkindi.
Awali katika homilia yake wakati wa Adhimisho hilo la Misa Takatifu, Paroko Msaidizi wa Parokia hiyo, Padri Nestory Damas, alisema kuwa mtu anayemshikilia Kristo, maisha yake yanakuwa ya thamani, bali anayejitenga na kuamua kumuacha Kristo, thamani yake inashuka na kupotea.
“Kumbe wapendwa, tunapomtafakari mwanapunda, na sisi twaweza kujifananisha kama mwanapunda. Unapokuwa na Yesu, unapokuwa na Kristo katika maisha yako, unakuwa ni mtu wa thamani, unakuwa ni mtu wa kipekee….
“Lakini pale ambapo unamuacha Kristo, basi thamani yako inashuka, thamani yako inapotea, na hasa pale ambapo tunamuacha tunafuata njia ambazo zinaelekeza kwenye giza, njia ambazo zinaelekeza kwenye upotovu. Kumbe leo tunatafakari kadri ambavyo tumesikiliza historia ya mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo, tujiulize swali moja ambalo litakuwa ni la tafakari yetu ya siku ya leo, ni nani alimuua Yesu?” alisema Padri huyo.
Aliwataka Waamini kuendelea kuyakabidhi maisha yao mikononi mwa Mungu, kwani ni yeye pekee ndiye mwenye maamuzi juu ya maisha yao.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.