Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kompany avurugwa na Waamuzi EPL

BURNLEY, Uingereza
Meneja wa klabu ya soka ya Burnley Vincent Kompany amelalamikia kiwango cha mwamuzi katika Ligi Kuu ya England msimu huu, akidai kuwa hakijakuwa kizuri vya kutosha.
Kompany alionyeshwa kadi nyekundu na mwamuzi Darren England wakati wa sare ya 2-2 dhidi ya Chelsea Jumamosi kwa kupinga uamuzi wa penati uliosababisha beki Lorenz Assignon kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Wachezaji sita wa Burnley wametolewa nje kwa kadi nyekundu katika mechi 30 msimu huu, idadi kubwa zaidi kuliko ya timu yoyote ya Ligi Kuu England.
Assignon alionyeshwa kadi ya pili ya njano muda mfupi kabla ya kipindi cha mapumziko kwa kumchezea vibaya Mykhailo Mudryk, na Kompany alitolewa uwanjani kwa majibu yake.
Burnley walitoka nyuma mara mbili dhidi ya Chelsea, huku Dara O’Shea akifunga bao la kusawazisha dakika ya 81 na kupata pointi moja.
“Nimewaambia waamuzi nimesema kwa njia ya kujenga, kuelewa na ukweli sio rahisi kwao”, alisema Kompany.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.