Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Julio awazodoa wapinzani wa Singida FG

Kocha Julio. Kocha Julio.

Dar es Salaam

Na Nicolaus Kilowoko

Kocha Mkuu wa klabu ya soka ya Singida Fountain Gate FC, Jamhuri Kihwelo maarufu kama ‘Julio,’ amepinga madai ya wachezaji wake kushuka viwango, na kueleza kuwa wanaoendelea kuisema timu hiyo, hawako sahihi.
Julio aliyaeleza hayo wakati akifafanua hali ya kambi na maandalizi ya timu yao kwa ajili ya mechi zijazo ambazo zipo mbele yao, ikiwemo mechi muhimu ya Ligi dhidi ya timu ya soka ya Yanga.
Alisema kuwa watu hawaijui klabu hiyo hiyo kuwa kwa sasa imebadilika, tofauti na huko nyuma kabla ya yeye hajaichukua, na kudai kuwa timu ina wachezaji wenye uwezo mkubwa wa kukupa matokeo chanya.
Julio alisema kuwa watu wamekuwa wakiisema vibaya klabu hiyo kuwa imelegalega, kitu ambacho siyo kweli kutokana na kuwa amekuwa na wachezaji wenye kujua nini wanafanya, tofauti na mitazamo ya watu wengine.
“Vijana wangu kwa sasa wanafanya mazoezi makubwa sana, hata ukiwaangalia, wanacheza kwa maelewano makubwa, na kwa asilimia 80 timu imebadilika sana kutokana na kuwa na wachezaji ambao wanajua nini wanachokifanya”, alisema Julio.
Alisema pia kuwa mbali na kuendelea kupambana nao katika mazoezi na kuwapa mbinu nyingi za kiufundi, lakini kitu kingine ambacho anendelea nacho kwa sasa ni kurekebisha ufahamu wao ili kuwajenga na kuwa bora kwa michezo yao ijayo.
Timu hiyo iliweka kambi Bamba Beach jijini Dar es salaam baada ya Ligi kusimama kwa muda, na hivyo kupelekea uongozi wa klabu hiyo wa kushirikiana na benchi la ufundi kwa ajili ya kuongeza kitu kwenye uchezaji wao.
Singida Foutain Gate wanatarajia kuwa na kibarua kizito Aprili 14 watakapokutana dhidi ya klabu ya soka ya Yanga katika mchezo wao wa Ligi mara baada ya kukutana na dhahama ya kipigi katika mchezo wao wa mzunguko wa kwanza wa Ligi.
Ikumbukwe hivi karibuni kwamba uongozi wa klabu hiyo ulifanya mabadiliko makubwa mara baada ya kuvunja benchi lote la ufundi la awali, na kumuajiri Kocha Jamhuri Kihwelo (Julio) ambapo lengo kuu ni kuinusuru timu hiyo isishuke daraja, bali kuleta sura mpya na mbinu mpya za kiufundi ili kufikia malengo yao ya msimu wa mwaka 2023/24.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.