Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kitabu cha Maisha ya Papa Benedikto XVI hadharani

VATICAN CITY, Vatican
Kitabu kuhusu maisha ya Baba Mtakatifu Benedikto XVI (2005-2013:wa 265-hayati), kimewekwa hadharani baada ya matayarisho yake kukamilika.
Kitabu hicho kinachofahamika kwa jina la El Sucesor, ikiwa na maana “Mtangulizi”cha mahojiano kati ya Papa na mwandishi Javier Martínez-Brocal, ambapo Papa Fransisko (2013 hadi sasa-wa 266)anamkumbuka Mtangulizi wake Papa mstaafu Benedikto XVI kuwa:”Daima alinitetea, na kamwe hakuniingilia.”
Papa Benedikto XVI alikuwa mtu mkuu kwa upole. Katika kesi nyingine baadhi ya watu walimtumia, labda bila ubaya, na walipunguza harakati zake. Kwa bahati mbaya, kwa maana nyingine, walikuwa wanamzunguka. Alikuwa ni mtu nyeti sana, lakini hakuwa mdhaifu, alikuwa mwenye nguvu.
Lakini kwake mwenyewe alikuwa mnyenyekevu, na  alipendelea kutojilazimisha. Kwa njia hiyo aliteseka sana. Haya ni baadhi ya meneno ambayo Papa Fransisko anayakumbuka ya Mtangulizi wake Benedikto XVI, katika kitabu cha mahojiano na Mwandishi Javier Martínez-Brocal (“El Sucesor”, Editorial Planeta), kitakachochapishwa Jumatano tarehe 3 Aprili, 2024.
“Aliniacha nikue na alikuwa na uvumilivu”, anaeleza Papa Fransisko. Na ikiwa aliona jambo lisilo sawa, alikuwa anafikiria mara tatu, au mara nne kabla ya kuniambia. Aliniacha nikue na alinipatia uhuru wa kuchukua uamuzi. ” Papa amesimulia, uhusiano ambao alifanya uzoefu wa karibu ya miaka 10 ya kuishi mjini Vaticani, na Papa Mstaafu kwamba: “Aliniacha huru, na hakuniingilia kamwe.”
Katika fursa ambayo kulikuwa na maamuzi ambayo hakuelewa, aliniomba maelezo kwa namna ya kawaida kabisa. Alinieleza: “Tazama sikuelewa hilo, lakini maamuzi yako mikononi mwako,” na mimi nilimweleza sababu, na yeye alifurahi.” Papa Fransisko katika kitabu ameeleza kwamba mtangulizi wake kamwe  hakuwahi kupinga uamuzi wake wowote kwamba: “Hakuwahi kuniondolea msaada wake. Labda kulikuwa na jambo ambalo hakulikubali, lakini hakulisema kamwe.”
Papa Fransisko aidha, alikumbuka wakati mwingine hata katika kumuaga Papa Mstaafu  Benedikto XVI, Jumatano tarehe 28 Desemba mwaka 2022, alipomuona kwa mara ya mwisho kwamba: “Benedikito alikuwa amelala kitandani. Alikuwa bado na fahamu, lakini alishindwa kuzungumza. Alinitazama, alinishika mkono, alikuwa anaelewa kile ambacho ninasema, lakini hakuweza kueleza neno lolote. Nilibaki kwa muda kitambo, kwa kumtazama na kumshika mkono. Ninakumbuka kabisa macho yake mang’avu… Nilimwambia maneno machache kwa upendo, na nilimbariki.’’
Papa Fransisko amekumbuka na kusimulia kesi maalum ambazo alitetewa na Papa Benedikto XVI: “Nilipata mazungumzo mazuri sana na yeye wakati alipokuwa Kardinali, na nilikwenda kukutana naye kwa kushangazwa na maneno yake juu ya ndoa kwa wanandoa, ambapo yeye alikuwa wazi kabisa na wao.
Siku moja walifika nyumbani kwake ili kunishtaki mbele yake eti  nilihamasisha ndoa za mashoga. Papa Benedikito hakuwa na wasi wasi  kwa sababu alikuwa anajua kabisa kile ambacho mimi ninafikiri.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.