Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Uinjilishaji Barani Afrika chini ya Wareno

Vasco Da Gamma Vasco Da Gamma

Katika safu hii ya Chimba Chimba Historia ya Kanisa wiki iliyopita, tuliangazia jinsi Uislamu ulivyoteka Afrika ya  Kaskazini. Leo tunawaletea jinsi gani Ukristo ulivyoinjilishwa Barani Afrika chini ya Wareno. Sasa endelea....

(Sehemu ya kwanza)

Kanisa la Afrika mwaka 1500
Mwaka 1500, Kanisa Barani Afrika lilikuwa limedhoofika sana. Misri, ingawa Ukristo ulidumu, Kanisa lilifanya kazi zake katika mazingira magumu sana, kwani waamini wake walinyanyaswa na Waislamu. Kila mwaka Wakristo wengi walihamia katika Uislamu.

Nubia sasa Sudan, ilipigana vizuri na kustahimili kwa miaka mingi lakini ufalme wake wa mwisho wa Alodia ulitekwa na Waislamu mwaka 1504 na polepole kufuta Ukristo wote.

Afrika ya Kaskazini inayojumuisha nchi za Tunisia, Libya, Algeria na Morocco, Ukristo ulitoweka kabisa chini ya utekaji wa Waislamu. Mfalme wa Ethiopia alikuwa amekimbilia milimani kwa sababu ya mashambulizi ya Waislamu, na ni kwa msaada wa Wareno mwaka 1543 ndipo alipoweza kujiimarisha tena.

Hivyo Ethiopia ikabaki nchi ya Kikristo hadi leo hii. Kusini mwa sehemu hizo zilizotajwa hapakuwepo na Ukristo. Ni katika hali hii ya Ukristo Afrika, tunaingia kipindi cha pili cha uinjilishaji chini ya Wareno.
                     
Misioni za Wareno Afrika (1400 – 1750)

Safari za Uvumbuzi:
Mhimili Mkuu wa uvumbuzi wa Ureno, alikuwa Mtoto wa Mfalme Henri Navigatores (1394-1460).  Mwaka 1415 aliteka Kisiwa cha Ceuto toka kwa Waislamu, na kwa mara ya kwanza Wareno walitawala bahari.  

Kutoka kisiwa hicho, alituma meli zake Kusini kwa uvumbuzi, licha ya simulizi za vitisho kwamba Kusini kuna mto wa moto, mtu atageuka mweusi, au kuna majitu makubwa wala watu.  Mafanikio ya safari hizo yalikuwa mazuri sana.  Kufikia  mwaka 1498 Vasco Da Gamma aliweza kuzunguka Afrika na kufika India.  

Kuna sababu kubwa zilizomtuma Henri na wenzake kufanya safari za utambuzi:

- Kwanza, ilikuwa ya kisayansi, alitaka kujua kulikoni huko Kusini.
       
- Pili, baada ya Ureno na Hispania kuwafukuza Waislamu kutoka nchi yao, walikuwa bado na mori ya vita vitakatifu. Walitaka kuwazunguka kupitia baharini na kuwashinda toka nyuma, kiasi kwamba wasingeliwasumbua tena.

Wakati huo palikuwepo simulizi nyingi juu ya ufalme wa Kikristo chini ya Mfalme Presta John. Walitumainia kuunganisha nguvu naye dhidi ya Waislamu. Wengi wanadhania kwamba ufalme huo ulikuwa ule wa Ethiopia.

- Tatu, ilikuwa sababu ya kibiashara. Walitegemea kugundua njia ya kufika India kupitia baharini. Kule kulikuwako na biashara ya dhahabu na vito ambavyo wangeliifanya bila kupitia nchi za Waislamu zenye hatari na ushuru mkubwa.
 
Vile vile waliona ugunduzi huu kama umisionari kwa ajili ya kuwainjilisha wapagani wa Afrika na Mashariki kwa ujumla.

Uinjilishaji na Udhamini wa Serikali (Padroado):

Toka mwanzo, Serikali ya Ureno ilidhamini na kusimamia shughuli zote za uinjilishaji.
Kila meli ya uvumbuzi iliyoanzia safari yake Ureno, ililazimika kuchukua Wamisionari.  

Papa Martin V mwaka1418 alizipa safari za ugunduzi hadhi ya vita vya msalaba kiasi kwamba walioshiriki safari hizo wote walipewa hadhi ya Kikanisa na neema zake.

Papa Callistus wa III mwaka 1456 aliwapa wafalme wa Ureno na Hispania madaraka ya Kikanisa ya kuanzisha majimbo na kuweka Maaskofu katika nchi zote walizozigundua.

Ingawa udhamini huu ulisaidia wamisionari kwenda misioni kwa bajeti ya serikali na ulinzi. Kuchanganya misioni na ukoloni pamoja na  biashara ilikuwa hatari sana.  

Mwishowe hali hiyo ilichangia sana kushindwa kwa missioni za Ureno Barani Afrika. Sasa nchi hizo zilikuwa na ukiritimba wa kuwatuma wamisionari wao katika nchi hizo watakaoweza kulinda maslahi ya taifa lao.

Vilevile kama wenyeji waliichukia serikali ya Ureno na ukoloni wake, vilevile walichukia wamisionari na imani ya Kikristo waliyoihubiri.

 Uinjilishaji Afrika ya Magharibi:

(a) Visiwa:
Visiwa vilikuwa rahisi kuinjilisha kwa sababu visiwa vingi hapakuwepo watu, na hivyo Wareno waliingia humo ambao tayari walikuwa Wakristo na kuwaleta watumwa waliofuata dini ya mabwana wao.

Visiwa vya Canary viligunduliwa na Hispania mwaka 1433.  Kule walipelekwa Mapadre Wafransiskani. Vilikaliwa na makaburu wa Hispania pamoja na watumwa ambao kwa kuoana waliingizwa katika utamaduni wa Hispania.

Ingawa visiwa hivyo viko Afrika, bado hadi leo ni sehemu ya Hispania. Wakazi wake ni wachache zaidi ya milioni moja, na na asilimia 80 ni Wakatoliki.
       
Visiwa vya Azores and Madeira viligunduliwa na Wareno mwaka 1420 na kukaliwa na wao pamoja na watumwa. Hadi leo ni sehemu ya Ureno, na asilimia 90 ni Wakatoliki.

Visiwa kumi vya Cape Verde viligunduliwa na Wareno mwaka 1460. Tofauti na visiwa vingine, hivi vilikuwa kwa ajili ya kulima pamba na miwa, na hivyo watumwa waliofanya kazi hiyo waliwazidi Wareno kwa wingi.

Hivyo mwaka 1975 walidai na kupata uhuru kama nchi ya Kiafrika licha ya kuwa na chotara wengi. Wakazi wake ni zaidi ya nusu milioni, asilimia 90 ni Wakatoliki.

Visiwa vya Sao Tome na Principe viligunduliwa mwaka 1470 siku ya Mtakatifu Tomaso, ndiyo sababu vikaitwa jina hilo. Sao Tome ilikuwa kituo maarufu kwa biashara na sukari. Askofu wake kwa miaka ya mwanzo alikuwa Askofu wa mwambao wote wa Afrika ya Magharibi.

Kisiwa kiliinjilishwa na watumwa huru kutoka Ureno. Mwaka 1975 pamoja na koloni nyingine za Wareno, kilidai na kupata uhuru wake. Kikiwa na wakazi 133,000 huku asilimia  88  wakiwa ni Wakatoliki.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.