Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Neno ‘The Gunners’ la Arsenal lilipoibukia

Herbert Chapman Herbert Chapman

Dar es Salaam

Na Arone Mpanduka

Arsenal ilianza kama utani hivi pale kikundi cha wafanyakazi katika kiwanda cha kuzalisha zana za kivita cha Woolwich, walipoamua kuunda klabu ya soka mwishoni mwa mwaka 1886.
Klabu ikawa ikishiriki michezo huku ikijulikana kama Dial Square. Mchezo wao wa kwanza waliifunga timu ya Eastern Wanderers 6-0, tarehe Desemba 11 mwaka 1886.
Baada ya muda mfupi, jina likabadilishwa na kuwa Royal Arsenal, huku timu ikiendelea kushiriki katika michezo ya kirafiki na mashindano ya nyumbani kwa kipindi cha miaka michache iliyofuata.
Mwaka 1891 klabu ikawa ya kulipwa na kubadilisha jina na kuitwa Woolwich Arsenal, na hatimaye kujiunga na ligi ya soka mwaka 1893.
Baadae jina lilibadilika kutoka Woolwich Arsenal na kubaki Arsenal, ambalo jina lake la umaarufu ni ‘The Gunners’ (washika bunduki), wanaitwa washika bunduki kwa sababu ya kutokea kwenye kiwanda cha kuzalisha silaha.
‘Washika bunduki’ hao wakahamia Highbury mwaka 1913 kama timu ya Ligi Daraja la Pili. Baada ya Vita ya Kwanza ya Dunia (1914-1918), Arsenal wakapigiwa kura na kuingizwa katika ligi daraja la kwanza, iliyokuwa imeongezwa ukubwa, ambako wameendelea kudumu hadi leo.
Herbert Chapman (pichani) alichukua nafasi ya kuiongoza Arsenal mwaka 1925, na mwaka 1930 akaiwezesha kupata taji lao la kwanza kabisa pale walipoifunga Huddersield katika fainali ya kombe la FA.
Mwaka uliofuata Arsenal wakawa mabingwa kwa mara ya kwanza. Kati ya mwaka 1933 na 1935 timu ikaweza kunyakua ubingwa mara tatu mfululizo (hali ambayo imeweza kufikiwa tu na timu nne vigogo). Chapman alifariki katikati ya safari hiyo ya mafanikio akiwa tayari ni mtu wa historia kubwa klabuni.
Vita ya Pili ya Dunia ilikata mwendo kasi wa Arsenal. Lakini baada ya vita hivyo, Tom Whittaker akawa meneja na mafanikio zaidi yakafuata. Arsenal wakawa mabingwa 1947/48 na 1952/53; washindi wa kombe la FA 1950 na washindi wa pili 1952.
Mwaka 1986, George Graham aliyekuwa mchezaji katika kikosi kilichochukua ubingwa 1971, akawa meneja akichukua nafasi ya Don Howe. Siku njema zaidi zikafuata. Akaiongoza Arsenal kunyakua kwa mara ya kwanza kombe la ligi mwaka 1986/87 kwa kuifunga Liverpool katika fainali.
Miaka miwili baadae washika bunduki wakanyakua ubingwa wa ligi na goli maarufu la dakika ya mwisho kutoka kwa Michael Thomas na matokeo kuwa 2-0 ndani ya Anfield. Taji jingine ikawa mwaka 1990/91 wakiwa na kikosi kilichopoteza mchezo mmoja tu, wakijivunia ukuta imara wa mabeki wanne.
Vikombe zaidi vikafuata. Mwaka 1992/93 Arsenal ikawa klabu ya kwanza kuchukua vikombe vyote vya ligi ya England katika msimu mmoja.
Msimu kamili wa kwanza wa Arsene Wenger 1997/98 katika uwanja wa Highbury, ulishuhudia Arsenal kwa mara ya pili katika historia yake ikifanikiwa kunyakua vikombe vyote viwili; cha Ligi Kuu na FA, na kumwezesha kocha huyo Mfaransa huyo kuchukua tuzo ya Carling ya meneja bora wa mwaka.
Dennis Bergkamp akawa mwanasoka bora wa mwaka wa Chama cha Waandishi wa Habari za Soka (FWA) na mwanasoka bora wa mwaka wa Chama Cha Wanasoka wa Kulipwa (PFA). Msimu huo uling’ara zaidi kwa wanasoka wa Arsenal kutoka Ufaransa Emmanuel Petit na Patrick Vieira, baada ya kutoa mchango wao mkubwa katika ushindi wa timu yao ya taifa katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 1998.
Msimu wa 2003/04 Arsenal wakamaliza michezo yote bila ya kufungwa na kuchukua taji la ubingwa wa Ligi. Pia walimaliza michezo yote wakiwa pointi 11 mbele ya mshindi wa pili Chelsea na kubeba taji kwa mara ya 13.
Tangu hapo Arsenal hawakupata mafanikio yoyote makubwa, na msimu wa 2022/2023 almanusura watwae taji la EPL, lakini walizidiwa kete na Manchester City.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.