Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Mtibwa yapiga teke wachezaji wageni

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Klabu ya soka ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imesema kwamba haina tena mpango wa kuwa na wachezaji wa kigeni,  kwa sababu hawana tofauti na uwezo walionao wachezaji wazawa.
Akizungumza na Tumaini Letu kwa njia ya simu kutoka Turiani Morogoro, Afisa Habari wa Klabu hiyo Thobias Kifaru alisema kuwa msimu uliopita walikuwa na wachezaji wa kigeni wasiopungua watano kutoka nchi mbalimbali Barani Afrika, lakini hawakuwasaidia chochote.
Alisema kwamba hata makocha watakaowatumia msimu ujao, ni wale wazawa pekee, kwa sababu wageni nao hawakuwa na mchango katika timu hiyo.
“Zamani tulikuwa na mfumo wa kutumia wachezaji wazawa, na kwa hakika tulifanikiwa kwa kiasi kikubwa, lakini baadae tukaona tujaribu kutumia mfumo wa wachezaji wa kigeni. Lakini sasa tunaona hakuna umuhimu wowote wa kufanya hivyo. Wanatuingiza kwenye gharama kubwa za uendeshaji, ikiwemo kuwalipia vibali na mishahara mikubwa, halafu hakuna matokeo mazuri uwanjani,” alisema Kifaru.
Alisema pia kuwa wapenzi wa soka wajiandae kuiona Mtibwa isiyo na kocha wa kigeni wala mchezaji wa kigeni katika msimu ujao, na kwamba huo ndio utakuwa utaratibu wao kwa misimu mingine inayofuata.
Kuhusiana na hoja ya ukata kusababisha wachukue maamuzi hayo ya kusajili wazawa, Kifaru alikana akisema kwamba Kampuni ya Mtibwa ina pesa nyingi, isipokuwa imeamua kurejesha uzalendo kwa kutumia wazawa pekee katika timu yao.
“Kiwanda cha Mtibwa Sugar ni kikongwe sana na hakijawahi kufilisika, vivyo hivyo hata kwenye timu. Sisi tulianza kuonekana Ligi Kuu mwaka 1995 na hujasikia tukitembeza bakuli kwa watu kuomba mchango.Kama tungekuwa na maisha hayo, sasa hivi tusingekuwepo kwenye ulimwengu wa soka,” alisema.
Mtibwa kwa sasa ipo chini ya kocha Habib Kondo mara baada ya kuachana na kocha Salum Mayanga waliyekuwa nae msimu uliopita.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.