Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Straika mpya Yanga ni ‘Mkufunzi’

DAR ES SALAAM

Na Arone Mpanduka

Imeelezwa kwamba mshambuliaji mpya wa Yanga kutoka nchini Ghana, Hafiz Konkoni, ni mwalimu kitaaluma.
Hayo yalisemwa na mwandishi wa habari za michezo nchini Ghana, Evans Gyamera, wakati akizungumza na Tumaini Letu kwa njia ya simu kutoka jijini Accra.
Gyamera ambaye pia ni miongoni mwa wadau wakubwa wa soka nchini humo, alisema kuwa Konkoni, licha ya kulijua kandanda, pia ana taaluma ya ualimu aliyoipata katika Chuo cha Ualimu cha Tumu (Tumu Teachers Training College) kilichopo Upper West nchini humo.
Mwanahabari huyo alisema kuwa kwa sasa Konkoni ana Diploma ya Ualimu wa Shule, ingawa mwenyewe anapenda zaidi kucheza soka.
Alisema kwamba taaluma aliyopata inamsaidia kuwa na weledi wa kufahamu lugha mbalimbali na kuzungumza kwa ufasaha, kitu ambacho kinamfanya aelewe vyema maelekezo ya makocha mbalimbali wanaomfundisha uwanjani.
“Ni kijana mwenye nidhamu na anajua kucheza soka, ikiwemo kutunza mpira kwenye miguu yake usipotee kirahisi kwa kupokonywa na wapinzani.Yanga wamepata mchezaji mzuri ambaye ninaamini atawasaidia,”alisema Gyamera.
Alisema Konkoni ni mchezaji ambaye amepata bahati ya kuaminiwa na kocha wa timu ya taifa ya Ghana Chris Hughton ambaye alimuita kwenye kikosi cha timu ya taifa na kumuacha kinara wa mabao Abednego Tettey.
Ikumbukwe kwamba msimu uliopita wa Ligi kuu ya Ghana, Konkoni alimaliza akiwa na magoli 15 na pasi za mwisho za usaidizi kabla ya kufunga magoli (assists) 3, akiwa katika nafasi ya pili, goli moja nyuma ya mfungaji bora Abednego Tettey, wa klabu ya Bibiani Gold Stars.
Hafiz kabla ya kujiunga na Bechem ya Ghana, aliwahi kucheza soka la kulipwa katika timu za Alsancak Ye ilova na Baf Ülkü Yurdu, za Kaskazini mwa Cyprus.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.