Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Pool Tanzania yaalikwa China

Mashindano ya pool yakiendelea jijini Dar es Salaam. Mashindano ya pool yakiendelea jijini Dar es Salaam.

DAR ES SALAAM

Na Mwandishi wetu

Chama Cha Pool Tanzania (Tanzania Pool Association: TAPA) kimepata mwaliko kwa wachezaji binafsi kushiriki mashindano ya JOY Grand Masters Final yatakayofanyika kuanzia Machi 24 hadi 29 mwaka huu huko Qinhuangdao nchini China.
Katika mashindano hayo, Tanzania itawakilishwa na Melckzedeck Amadeus aliyemaliza kama mchezaji bora wa Bara la Afrika katika mashindano ya Afrika yaliyofanyika Afrika Kusini mwaka 2023.
Msemaji wa Chama hicho Akida Kilango alisema kuwa mchezaji atakayependa kushiriki katika mashindano hayo anaweza kupata fursa hiyo kwa kujigharamia nauli ya ndege kwenda na kurudi, malazi, pamoja na chakula.
Alisema kuwa mchezaji huyo atatakiwa kuwasiliana na TAPA ili kuweka mambo sawa juu ya ushiriki wake.
TAPA itamsaidia katika upatikanaji wa nyaraka muhimu ikiwemo mwaliko kwa ajili ya safari na itagharamia gharama ya kupata VISA.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.