Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Kidunda arejea na Mwafrika Kusini

DAR ES SALAAM

Na Nicolaus Kilowoko

Baada ya kukaa miezi saba bila kuwa na pambano lolote, bondia Suleiman Kidunda anatarajiwa kupanda ulingoni mwezi Machi mwaka huu dhidi ya bondia kutoka nchini Afrika Kusini.
Selemani Kidunda anatarajiwa kuzipiga dhidi ya bondia Asemahle Wellem kutoka Afrika Kusini katika pambano ambalo litapigwa Machi 1 mwaka huu katika ukumbi wa Warehouse, Masaki, jijini Dar es Salaam.
Kidunda alisema kuwa kimya kingi, kishindo huvuma, hivyo kwa sasa ameshaingia vitani kupambana na kukaa kwake pembeni kumemfanya aendelee kujifua dhidi ya mapambano yake huko mbele.
Bondia Asemahle Wellem kutoka Afrika Kusini ni sawa na mfupa uliowashinda wengi, kwani amekuwa na mapambano mengi na kuwashinda wengi katika mapambano yake.
“Mashabiki wangu naomba msiwe na hofu, dogo katangaza vita na mimi nishaingia vitani, yaani nimeshaingia chaka, nipo tayari kupambana, tuombe Mungu tukutane hiyo siku,” alisema Kidunda.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.