Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Ukraine yapewa mbinu kumaliza vita

VATICAN CITY

Baba Mtakatifu Fransisko amesema Serikali ya Ukraine inapaswa kukubali na kuwa jasiri katika majadiliano ya kusaka amani ya kudumu.
Alisema kuwa Ukraine haina budi kuonesha ujasiri na kuanza kujikita katika majadiliano ili kusitisha vita hiyo ambayo inaendelea kusababisha athari kubwa kwa maisha ya watu na mali zao.
Vita ya Ukraine, kuna baadhi ya nchi ambazo zimejitolea kuongoza majadiliano kati ya Urusi na Ukraine na kati ya nchi hizi na Uturuki, kabla ya mambo hayajawa mabaya zaidi. Lengo la majadiliano ni kuokoa maisha ya watu. Ukraine imeteseka tangu utawala wa Stalin.
Vita kati ya Urusi na Ukraine, Israeli na Palestina pamoja na athari zake kwenye Ukanda wa Gaza, ni kati ya tema zilizojadiliwa na Baba Mtakatifu Fransisko kwenye mahojiano maalum kati yake na Lorenzo Buccella wa Kituo cha Radio Na Televisheni cha Uswis, “Radiotelevisione Svizzera, RSI.” Mahojiano haya yatachapishwa rasmi tarehe 20 Machi mwaka 2024.
Katika mapambano dhidi ya Ugonjwa wa Virusi vya Korona, UVIKO-19, Kanisa limetumia silaha zifuatazo; Kufunga na kusali; Ibada ya Misa Takatifu; Tafakari ya Neno la Mungu; Matendo ya huruma; kiroho na kimwili pamoja na Rozari Takatifu, ili kuwajengea watu imani, matumaini na mapendo katika kipindi hiki kigumu cha historia, sanjari na kukimbilia faraja na wokovu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Machi 13 mwaka 2013 Baba Mtakatifu Fransiko alichaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki (Papa wa 266), kielelezo cha huduma na mwaliko wa kuchuchumilia utakatifu wa maisha, aligusia madhara ya vita, na kwamba Jumuiya ya Kimataifa haina budi kujikita katika kutafuta na kudumisha amani duniani, ili kuondoa giza la maisha linalomsonga mwanadamu sanjari na kuondokana na unafiki katika maisha, ili kutangaza na kushuhudia ukweli.
Baba Mtakatifu Fransisko alisema, Vita kati ya Urusi na Ukraine, Israeli na Palestina pamoja na athari zake kwenye Ukanda wa Gaza ni mambo yanayofifisha matumaini ya watu wa Mungu, na kwamba hili ni jambo baya sana na kwamba vita mara nyingi inahitimishwa kwa pande husika kuwekeana mkataba.
Baba Mtakatifu alitumia sura ya bendera nyeupe iliyopendekezwa wakati wa mahojiano ili kuonesha umuhimu wa kusitisha chuki na uhasama, ili hatimaye, kufikia maridhiano yanayopaswa kufikiwa kwa ujasiri katika mazungumzo, na kwamba matumaini yake ni suluhisho la kidiplomasia kwa haki na amani ya kudumu.
Baba Mtakatifu alikaza kusema kwamba Ukraine haina budi kuonesha ujasiri na kuanza kujikita katika majadiliano ili kusitisha vita hii ambayo inaendelea kusababisha athari kubwa kwa maisha ya watu na mali zao.
Kuna baadhi ya nchi ambazo zimejitolea kuongoza majadiliano kati ya Urusi na Ukraine, na kati ya nchi hizi na Uturuki, kabla ya mambo hayajawa mabaya zaidi. Lengo la majadiliano ni kuokoa maisha ya watu.
Ukraine ni taifa lililoteseka tangu utawala wa Joseph Stalin, kiongozi wa Sovieti ya Urusi.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Kanisa kwa miaka ya hivi karibuni, Baba Mtakatifu Fransisko aliadhimisha Ibada ya Liturujia ya Neno la Mungu, iliyoambatana na Ibada ya Kuabudu Ekaristi Takatifu pamoja na kutoa baraka kwa mji wa Roma na Ulimwengu katika ujumla wake, maarufu kama “Urbi et Orbi” kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican.
Baba Mtakatifu alibainisha Vita nchini Slovakia kuwa imewafuta wazee wengi, na kwamba hakuna picha kubwa zaidi ya madhara ya vita kama hii, kwani watu wengi wanafariki dunia, na kwamba Njiwa ni alama ya amani.
Vita kati ya Ukraine na Urusi vimesababisha madhara makubwa.
Baba Mtakatifu alisema kwamba watoto wengi anaokutana nao kutoka kwenye maeneno ya vita hawana furaha, amani na utulivu wa ndani; ni watu ambao kesho yao imepokwa. Vita daima ni kielelezo cha kushindwa ubinadamu.
Hakuna vita ya haki, bali vita ni matokeo ya biashara haramu ya silaha duniani, kielelzo cha watu wachache kujichumia utajiri wa haraka haraka kwa damu ya watu wasiokuwa na hatia. Hiki ni kielelezo cha giza katika maisha ya mwanadamu, ubinafsi unaoteketeza maisha ya watu kimaadili.
Kwa bahati mbaya mwanadamu katika maisha yake, anayo pia sehemu ya giza, kielelezo cha dhambi inayomwandama mwanadamu. Giza katika maisha ya mwanadamu linaweza kudumu kwa kitambo kirefu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.