Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Murray akataa kustaafu tenisi

Nottingham, England
Andy Murray anajiandaa kwa Wimbledon yake ya 15, itakayoanza Julai 3 mwaka huu, huku nyota huyo mwenye umri wa miaka 36, lakini hatazami kustaafu hivi karibuni.
Andy Murray anatumaini Wimbledon ya mwaka huu haitakuwa yake ya mwisho, akisema kwamba anataka kujituma kwa kucheza kwa kiwango cha juu sana kabla ya kutundika daluga lake.
Murray alitolewa katika robo fainali na Sam Querrey huko Wimbledon mnamo 2017, na kazi yake ilionekana kuwa mwisho baada ya kutolewa kwenye Australian Open mnamo mwaka 2019, lakini upasuaji wa kurekebisha nyonga yake ulimpa nafasi ya pili mchezaji huyo wa zamani wa Ulimwengu.
Ushindi wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 katika michuano ya hivi majuzi ya Nottingham Challenger, ulimpeleka kwenye cheo chake cha juu zaidi tangu upasuaji wake wa nyonga akiwa nambari 38 duniani.
Murray aliorodheshwa katika nafasi ya 839 duniani mnamo Julai 2018 alipopata nafuu baada ya upasuaji wake wa kwanza wa nyonga, kushindana na Grand Slams tena kulionekana kuwa tumaini la kusikitisha, lakini amepambana, na sasa ana matumaini makubwa ya kushindana tena katika daraja la juu la mchezo huo.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.