Login to your account

Username *
Password *
Remember Me

Create an account

Fields marked with an asterisk (*) are required.
Name *
Username *
Password *
Verify password *
Email *
Verify email *
Captcha *
Reload Captcha

Whyte ataka pambano la marudiano na AJ

LONDON, England
Dillian Whyte yuko tayari kwa mechi ya marudiano na mpinzani wa uzito wa juu wa Uingereza, Anthony Joshua, katika ukumbi wa O2 Arena, Agosti 12 mwaka huu, lakini kifungu cha marudiano ya pambano hilo, ni mazungumzo magumu.
Whyte ambaye ni mwana masumbwi mahiri na alimshinda Joshua, kabla ya AJ kumshinda mwaka 2015 na sasa Whyte bado anataka nafasi ya kulipiza kisasi hasara hiyo.
Whyte alianza tena mazungumzo wiki jana baada ya kumpinga kwa maneno promota Eddie Hearn kuhusu kukatika kwa mawasiliano kuhusu mechi ya marudiano inayotarajiwa kuwa kubwa, ambayo inatarajiwa kuandaliwa katika uwanja wa The O2 mnamo Agosti 12.
Whyte ana ushindani wa muda mrefu na Joshua na alimshinda AJ kama mwanariadha, kabla ya Joshua kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki huko London mwaka 2012.
Na Joshua tayari amekuwa akihusishwa na pambano linalotarajiwa kupigwa na Deontay Wilder, litakalofanyika Mashariki ya Kati baadaye mwaka huu.

Rate this item
(0 votes)

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.